Baada ya hayo matokeo watu wengi ana walitamani kumfahamu huyu
mwanafunzi, Jina lake la kuzaliwa ni Julius lakini la kisanii ni
Elinaja, na ametoa sababu 5 za kwa nini aliamua kuandika hiyo mistari ya
bongo fleva kwenye mitihani yake ya kumaliza kidato cha nne.
Amesema “1 ni kutaka kutuma ujumbe kwa watu wanaosimamia Elimu kwa
ujumla, sababu ya pili ni kutaka kusaidia watu wanaoteseka mtaani ambao
wanaishi maisha magumu kwa sababu tu ya kushindwa kwendana na system ya
elimu iliyopo ambayo ukishindwa kwenda nayo sawa umefeli, tulivyoumbwa
kuna mtu anaweza akawa anashindwa kitu flani lakini ni mzuri kwenye kitu
kingine sasa mfumo uliopo hautoi nafasi kwa wasioweza hiyo system,
sababu ya tatu ni kutokana na utaratibu wa usaishaji wa mitihani kwa
sababu sijui kama kuna mwanafunzi yeyote aliewahi kufanya mtihani wake
wa mwisho alafu mtihani wake ukarudishwa ili kuona wapi alipokosa na
wapi alipopata”
“Sababu ya nne ni kuhusu wazazi kutambua uwezo wa watoto wao toka
wakiwa wadogo kipi wanaweza kipi hawawezi ili kuokoa muda na pesa,
sababu ya tano ni kwa serikali ijaribu kuweka shule za vipaji toka
mwanafunzi akiwa mdogo kabisa, leo hii kuna mtu amepata degree pale chuo
kikuu kasoma miaka mitatu na kupewa degree ya sanaa lakini hawezi
kukuonyesha cheti hata kimoja kwamba alikua na elimu ya awali ya hiyo
degree, huwezi kuniambia una degree wakati hukupata elimu ya msingi ya
ulichosomea”
“Kwa namna moja au nyingine sidhani kama nimefanikiwa kwa sababu
nilichofanya watu walikichukulia tofauti sikufanikiwa ndio maana
nimeamua kujitokeza kumalizia kazi ambayo niliianza kuifanya kule kwa
sababu nafsi yangu ilikua inanisuta, ila kwa sasa watu watakua wameelewa
na ninaweza kuwasaidia watu wengine” – Julius (Elinaja)
No comments:
Post a Comment