Monday, April 30, 2012

TASWIRA ZA DIAMOND PLATINUM ALIVYOTUA NA CHOPER NDANI YA DAR LIVE HAPO JANA


Huyu ndiye Diamond mwingine hakunaga, akielekea kupanda helikopta kwenda viwanja vya Dar Live kufanya makamuzi jana Jumapili, 29 April 2012
Diamond akiwa na rubani wake wakielekea kwenye helikopta
Hapa nimemkubali maana hakuna kitu muhimu kama kujikabidhi mikononi mwa Mungu kabala ya kufanya jambo lolote
Helikopta ikingia uwanjani hapo chezeaaa
Dar Live palikuwa hapatoshi
Helikopta ikamshushua ka kuondoka zake
Diamond akimsalute rubani wake na Mwenyezi Mungu kwa kumfikisha salama
 Nimpende nani? Nimpende nani? hahaha nawaza kwa sauti tu

 full mzuka
 Mambo ya mavazi ya Diamond na dancers wake naona yalikuwa ni mwendo wa US Marine Style.SOURCE: lukaza

MBUNGE WA SUMBAWANGA MJINI (CCM) AVULIWA UBUNGE NA MAHAKAMA

Hukumu ya kupinga matokeo ya ubunge wa sumbawanga mjini wa Aeshy Hilaly Halphany CCM dhidi ya mwalimu Norbet Joseph Yamsebo wa Chadema ambaye anadai kuchakachuliwa katika uchaguzi huo.

Madai miongoni ni pamoja na kutoa rushwa kwa makundi mbalimbali na watu wengi walijitokeza kutoa ushahidi huo na kukiri kuwa ni kweli walipokea vitu mbalimbali ikiwemo fedha, baskeli, pikipiki, vinywaji, kinanda kwa kanisa katoliki, nk kwa sharti la kumpigia kura mbaya zaidi ni kwa mkurugenzi mwanamama kutoa ushahidi wa kupinga ushindi wa mbunge huyo, mkurugenzi huyo alihamishwa muda mfupi mara baada ya matokeo ya uchaguzi kutolewa na kupelekwa wilaya ya Ileje.

Kwa mujibu wa taarifa za kuaminika. Mahakama imemvua ubunge mbunge wa CCM Bw. Aheshy Hilal. 
Habari zaidi tutawaletea tembelea my tanzania. Kwa hisani ya lukaza

Sunday, April 29, 2012

MAMIA WAJITOKEZA KWAAJILI YA SHOW YA WASHINDI WA KILI MUSIC AWARDS 2012 NDANI YA UWANJA WA JAMHURI MKOANI DODOMA


Mamia ya Wananchi wakiwa kwenye foleni tayari kuingia ndani kwaajili ya Show ya washindi wa Kili Music Awards ilofanyika katika uwanja wa jamhuri mkoani Dodoma jana

Mshindi wa Kilimanjaro Star Search Issa akiwa Jukwaani huku akishusha burudani kwa wapenzi wa Muziki wakiojitokeza kushuhudia Tamasha kubwa la Washindi Wa Tuzo za Kili Musics Awards 2012
Mshiriki wa Shindano la Kili Star Search akitoa Burudani katika show ya Washindi Wa Kili Music Award 2012 katika Uwanja wa Jamhuri Mkoani Dodoma 
Kutoka Kulia ni Mshindi wa Kwanza wa Kilimanjaro Issa Kutoka Pande za UDOM na Mshiriki wa BSS 2008 ameshinda kwenda kurekodi nyimbo zake na gharama hizo zitalipwa na Kilimanjaro, wa pili ni Juma na Mwisho ni Alice
Issa Mshindi wa Kwanza wa Kili Star Search akipongezana na Mshindi wa Pili wa Kili Star Searc 2012 katika Show ya washindi wa Tuzo za Kili zilizofanyika katika uwanja wa Jamhuri Mkoani Dodoma

Saturday, April 28, 2012

KAMATI KUU YA CCM YAMRIDHIA RAIS KUVUNJA BARAZA LA MAWAZIRI.

MWENYEKITI WA CCM RAIS JAKAYA KIKWETE ALIPOONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU.



MWENYEKITI WA CCM RAIS JAKAYA KIKWETE AKIONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU  IKULU DAR ES SALAAM.(PICHA NA IKULU).

TASWIRA ZA TUNDU LISSU BAADA YA KUIBUKA KIDEDEA KESI YA UBUNGE SINGIDA MASHARIKI.


Wakili wa waleta maombi Wanaccm Godfrey Wasonga akitafakari kwa hisia kali muda mfupi kabla ya kesi ya kupinga matokeo yaliyompa ubunge Tundu Lissu hayajatangazwa.
Mbunge wa jimbo la Singida mashariki CHADEMA),Tundu Lissu,muda mfupi baada ya mahakama kuu kutupilia mbali maombi yaliyotolewa na Shaban Selema na Pascal Halu wa CCM,kupinga matokeo yaliyompa ushindi wa ubunge.
Mbunge wa jimbo la Singida mashariki (CHADEMA) Tundu Lissu akifutwa machozi na mke wake wakati wakitoka nje ya mahakama baada ya mahakama kuu kutangaza kuwa ushindi wake huo,ni halali.
Baadhi wa watu waliohudhuria kusikiliza kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi yaliyompa ushindi Tundu kuwa mbunge muda mfupi baada ya maamuzi hayo kutolewa.(Picha zote na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu.
Mbunge wa jimbo la Singida mashariki (CHADEMA)Tundu Lissu imeigaragaraza vibaya CCM baada ya mahakama kuu kutupilia mbali hoja 11 zilizowasilishwa na waleta maombi wawili wanachama wa CCM za kutaka kutengua ushindi wake wa ubunge kwa madai kuwa, alikiuka sheria na taratibu za uchaguzi na kusababisha uchaguzi huo kutokuwa huru na wa haki.
Shabani Selema na Pascal Halu wote wanachama wa CCM na wakazi wa kijiji cha Makiungu tarafa ya Mungaa jimbo la Singida Mashariki, walifungua kesi ya kupinga matokeoa yaliyompa ushindi Tundu kwenye uchaguzi mkuu uliopita.
Jaji Mosses Mzuna wa makahama kuu Moshi mjini mkoa wa Kilimanjaro, katika kutoa hukumu hiyo, amesema ushahidi uliotolewa na upande wa waleta maombi, umeshindwa kuthibitisha bila kuacha shaka yo yote kuwa, mlalamikiwa wa kwanza, wa pili mwanasheria mkuu wa serikali na wa tatu msimamizi wa uchaguzi, kuwa walivunja/kiuka  sheria, taratibu na kanuni za uchaguzi na kusababisha uchaguzi huo kutokuwa huru na wa haki.
Akitoa maamuzi ya makahama, amesema kuwa katika hoja zote 11 zilizoletwa na waleta maombi hao, ushahidi wote ni wa kuhisi, kusikia  na kushuku, ambao hauna uhalisia wa mambo yaliyowasilishwa.
Jaji Mzuna amesema kuwa mahakama yo yote haiwezi kutegua matokeo ya uchaguzi kwa kuambiwa maneno matupu bila ya maneno husika kuthibishwa kwa ‘document’ husika.
Amesema ushahidi wa upande wa walalamikaji pia umekuwa ni kama kinyonga, mara kwa mara ulikuwa ukukigeuka geuka.
Akifafanua zaidi, Mzuna ametaja  baadhi ya hoja ambazo zililetwa na waleta maombi kuwa ni mlalamikiwa Tundu kuandaa barua tano zinazofanana kwa mawakala wa CUF, TLP, AAPT Maendeleo, NCCR -Magezui na CHADEMA, kwa lengo la kujinufaisha katika zoezi la uchaguzi mkuu.
Ametaja hoja nyingine kuwa Tundu aliwapa chakula mawakala wa chama chake na wa vyama vingine isipokuwa wa chama cha CCM, kitendo ambacho kiliashiria ni hongo ili mawakala wasiokuwa wa chama chake nao wampigie kura.Habari Kwa Hisani ya MO Blo

Thursday, April 26, 2012

Hukumu ya Charles Taylor leo

Majaji katika mahakama maalum kuhusu vita nchini Sierra Leone, leo watatoa hukumu dhidi ya aliyekuwa Rais wa Liberia Charles Taylor kwa kuhusika na vita hivyo vilivyodumu miaka 10.
Charles Taylor
Taylor anasema kesi hiyo ni njama ya kisiasa
Taylor anakabiliwa na mashtaka 11 ikiwemo ubakaji na mauaji ya raia wa Sierra Leone.
    Ikiwa atapatikana na hatia atakuwa rais mstaafu wa kwanza kuhukumiwa na mahakama ya kimataifa.
Kiongozi huyo wa zamani anadaiwa kufadhili waasi wa RUF.
Zaidi ya mashaidi 100 wamefika mbele ya mahakama hiyo lakini Bw Taylor amekanusha kuhusika na uhalifu huo wakivita na anadai kuwa kesi hiyo ni njama ya kummaliza kisiasa.
Hukumu ya majaji hao inasubiriwa kwa hamu sana na raia nchini Sierra Leone ambao jamaa zao waliathirika sana wakati wa vita hivyo.
Inakadiriwa kuwa zaidi wa watu elfu 50 waliuawa na wengine wakiwemo wanawake na watoto walibakwa na kukatwa mikono au miguu na waasi wa RUF ambao upande wa mashtaka unasema walipata usaidizi wa silaha kutoka kwa Bw Taylor.
Wakati wa vita hivyo, mwendesha mashtaka anasema kuwa Taylor alikuwa kiungo muhimu katika biashara haramu ya almasi kutoka Sierra Leone.
Kesi hii iliodumu miaka mitatu na nusu, hata hivyo huenda isi kamilike leo kwani pande zote wanauhuru wa kukata rufaa ikiwa hukumu hiyo haitawaridhisha.

Wednesday, April 25, 2012

Ni Maafa,Ubakaji, na Uasi DRC


Wanajeshi wa DRC wakimpa buriani mwenzao.

habari kutoka Mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo zinasema mapigano makali kati ya wanajeshi na waasi yamesababisha ubakaji wa halaiki na mauaji ya wanajeshi tisa.
Duru zinasema zaidi ya watu 100 wamebakwa katika eneo la Mweso lililoko Kivu ya Kaskazini. Zaidi ya raia elfu 80 wamaaninika kukimbia mapigano hayo ambapo pia kuna taarifa za wanajeshi 20 wa serikali kuasi.
Walioasi wanaaminika kuwa waaminifu kwa jenerali muasi Bosco Ntaganda anayetakikana na mahakama ya Kimataifa ya jinai-ICC. Ntaganda ameshtakiwa kwa makosa ya uhalifu wa kivita ambapo anatuhumiwa kuwasajili watoto jeshini.  habari kwa msaada wa BBC SWAHILI.COM

Tuesday, April 24, 2012

Wabunge, Serikali sasa jino kwa jino



Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe
WATUPA MPANGO WAKE WA MAENDELEO, PIA WAJIPANGA KUKWAMISHA BAJETI, CHADEMA WAANDAA MAANDAMANO
Daniel Mjema, Dodoma na Editha Majura, Dar
KITENDO cha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kushindwa kuzungumzia shinikizo la baadhi ya wabunge kutaka mawaziri wanane wajiuzulu, kimeonekana kuwakera wawakilishi hao ambao sasa wameamua kuibana Serikali huku wakiapa kukwamisha bajeti za mawaziri hao katika Bunge lijalo la Bajeti.Jana walianza kuonyesha makali baada ya kukataa mapendekezo ya Mfumo wa Mpango wa Mabadiliko wa Maendeleo wa Taifa kwa mwaka 2012/2013 wakisema hauna jipya na umetayarishwa kwa mfumo uleule kwa miaka 15 mfululizo.

Juzi, Pinda aliahirisha Bunge bila kugusia shinikizo la wabunge hao kutaka Serikali iwawajibishe Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo; Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja; Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu; Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Cyril Chami; Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hadji Mponda; Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Profesa Jumanne Maghembe; Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), George Mkuchika.
Wakizungumza na kwa nyakati tofauti jana, wabunge hao, wengi wao wakiwa ni wa CCM, walisema silaha pekee waliyobaki nayo ni kukwamisha Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2012/2013 katika kikao kijacho cha Bunge.
Wabunge hao pia wameonya kwamba kutojiuzulu kwa mawaziri hao kutaiweka CCM njia panda katika Uchaguzi Mkuu wa 2015 kwani hoja ya ufisadi ndiyo iliyowafanya wenzao wengi wasirudi bungeni.
“Silaha kubwa tuliyobaki nayo sasa ni kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu na nakuambia kama ile karatasi ingerudi upya leo idadi ya wabunge wa CCM ambao wangetia saini ingetikisa nchi,” alisema James Lembeli wa Kahama (CCM).
Lembeli alisema anashangaa kuona mawaziri waliotakiwa kujipima wenyewe na kuandika barua za kujiuzulu wakigoma kufanya hivyo na Serikali kupuuza hoja hiyo akisema, hatashangaa kuona Watanzania wakiingia mitaani.
“Kitendo cha Waziri Mkuu kutosema chochote kuhusu kujiuzulu kwa mawaziri hao wakati akihitimisha Bunge ni kuiingiza nchi kwenye mgogoro mkubwa. Serikali ifahamu kuwa, ipo madarakani kwa ridhaa ya wananchi,” alisema.
Lembeli alisema wananchi walipokea kwa shangwe taarifa ya mawaziri hao kutakiwa kujiuzulu lakini, kitendo cha Waziri Mkuu kuwaacha na kuikwepa hoja hiyo alipokuwa akiahirisha Mkutano wa Bunge juzi, kitaongeza chuki ya wananchi dhidi ya Serikali yao kwa kuwa wataamini inawakumbatia mafisadi.
“Inakuwaje hawa mawaziri wanane tu watake kuitumbukiza nchi kwenye machafuko? Uwaziri ni dhamana aangalie huko kwenye vijiwe na mitaani watu walivyoshangilia kusikia wametakiwa kujiuzulu leo wanagoma, unamgomea nani?” alihoji Lembeli.
Lembeli alisema anaamini Rais atafanya uamuzi mgumu na wa haraka kabla ya Bunge la Bajeti vinginevyo Waziri Mkulo na mawaziri wengine watakuwa na wakati mgumu ambao haujawahi kuonekana katika kupitisha bajeti za wizara zao.
Mbunge mmoja wa Viti Maalumu kwa tiketi ya CCM kutoka Kanda ya Ziwa, alisema ukimya wa Rais Kikwete na kiburi cha mawaziri wake wenye tuhuma za kweli kugoma kujiuzulu, kumezidi kukifanya chama hicho tawala kuporomoka umaarufu.

Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe (CCM), alisema Rais Kikwete anapaswa kuheshimu maoni na maelekezo ya wabunge na kusema hata kutaka mawaziri wajiuzulu ni utaratibu tu wa kistaarabu.
“Sisi Wabunge 76 tuliosaini hoja ya kutaka Waziri Mkuu ang’oke tumejitoa sadaka kwa maslahi ya nchi lakini naamini wakati wa kumpigia kura Waziri Mkuu, wengi zaidi watatuunga mkono kwa jinsi walivyokerwa na jambo hili,” alisema.
“Bunge safari hii limeisha kimyakimya, Spika alipowahoji wanaoafiki hoja ya Waziri Mkuu ya kuliahirisha Bunge waliosema siyo ndiyo waliokuwa wengi na kama ulifuatilia Bunge lilikuwa kimya si kawaida… Rais anatakiwa alione hilo,” alisema.
Mbunge wa Kinondoni, Iddi Azzan (CCM), alisema amesikitishwa na hatua ya mawaziri hao kugoma kujiuzulu na kwamba kwa hali ilivyo, busara ya kawaida inataka mawaziri hao wajiuzulu.
“Kwa busara ya kawaida wote wanaotuhumiwa kwa wizara zao kufanya madudu wangeacha uroho wa madaraka na kujiuzulu ili kuitikia kilio cha wabunge na Watanzania kwa sababu upepo huko nje sio mzuri hata kidogo,” alisema Azzan.
Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) alisema taifa limeghafilika kwa sababu wananchi wengi nchi nzima walikaa kwenye luninga na kusikiliza redio juzi jioni wakitarajia Waziri Mkuu angetamka moja kwa moja kuwang’oa mawaziri hao.
“Jana kwenye baa na vijiwe ilikuwa kama vile kuna mechi ya kukata na shoka... kwa jinsi idadi kubwa ya wananchi walivyofuatilia hotuba ya Waziri Mkuu lakini mwisho wa siku akawaacha solemba,” alisema.
Nape, Mukama

Baadhi ya wabunge wa CCM waliosaini barua ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu wamedai kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho Wilson Mukama amewatisha.

Kanji Lugola wa Mwibara alidai jana kwamba usiku wa kuamkia Jumapili, siku moja baada ya kusaini hati hiyo alipokea simu kutoka kwa Mukama akimtolea maneno makali kutokana na hatua yake hiyo.

“Alizungumza maneno mengi ya vitisho kwa mfululizo bila hata kunipa nafasi ya kujieleza, akasema, ‘nakuja huko wewe na huyo mwenzako mliosaini mtanitambua,’ kuona hivyo tukaondoka Dodoma usiku huohuo,” Lugola alieleza.

Alisema walisafiri hadi Dar es Salaam na kwamba walihudhuria kikao cha Bunge cha Jumatatu iliyopita wakitokea mafichoni.Alipotakiwa kuthibitisha madai hayo Mukama alisema: “Siwezi kutoa habari kwa simu.”

Alipopigiwa tena na kuombwa afuatwe ofisini alisema, “Kwa leo haitawezekana maana niko njiani natokea Dodoma sasa hivi nimefika Gairo, kama unaweza njoo kesho.”

Lugola alidai wakati akipokea vitisho hivyo kutoka kwa Mukama waliokuwa wamesaini kwa upande wa CCM walikuwa yeye na Filikunjombe, baadaye alifuatia na Nimrod Mkono.

“Kinachofanya tufikie hatua hii ni kutoridhishwa na dhamira ya dhati ya chama chetu katika kuisafisha Serikali… na ieleweke kuwa hatuna mpango wa kuhama chama chetu kwa kuwa lengo letu ni kukiimarisha,” alisema.

Akizungumzia madai hayo ya vitisho, Katibu wa Uenezi na Itikadi wa CCM, Nape Nnauye alisema wabunge hao hawana hatia kwani msimamo wao ni sehemu ya kutekeleza wajibu wao.

Alisema ingawa hakuwa na taarifa za vitisho dhidi ya wabunge hao, CCM hakijafanya kikao chochote kuzungumzia suala hilo na kusema kama kuna mtu aliyewatisha basi amechukua hatua zake binafsi.

“Wabunge wana haki ya kuhoji utendaji wa Serikali yao na hata kuiwajibisha, hakuna mwenye haki ya kuwabagua kiitikadi, kiimani wala kikabila hivyo wanaojadili suala hili kwa misingi ya kibaguzi hawawatendei haki…, wanataka watekeleze vipi majukumu yao?”

Alisisitiza kuwa ndiye msemaji wa CCM hivyo ieleweke kuwa kilichofanywa na wabunge si uasi na jamii isiwagawe kwa namna yoyote ile bali, matendo yao ndani ya Bunge yaheshimike kwa mujibu nyadhifa zao.

Waanza kuonyesha makali
Wabunge waliyakataa mapendekezo ya Mfumo wa Mpango wa Mabadiliko wa Maendeleo wa Taifa kwa mwaka 2012/2013 wakisema hauna jipya na umetayarishwa kwa mfumo uleule kwa miaka 15 mfululizo na kwamba vigezo vyote, uchumi wa Tanzania unakuwa kwa viwango visivyoridhisha na ukuaji huo hauendi sambamba na kasi ya kupunguza umasikini na kukuza pato la mwananchi wa kawaida.

Mpango huo ulioandaliwa na Tume ya Mipango kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha uliwasilishwa jana kwenye Kamati ya Mipango ya Bunge na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira.

Akiwasilisha maoni ya Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Dk Abdallah Kigoda alisema mfumo huo unahitaji mabadiliko ili uendane na wakati uliopo ikiwamo kutoa majibu ya tatizo la mfumuko wa bei.

“Mapendekezo yanayotayarishwa yanajikita zaidi kwenye eneo la maelekezo badala ya maagizo. Lazima Serikali itoe majibu kuwa sera za fedha na kodi zinatakiwa ziweje ili kujibu tatizo la mfumuko wa bei na kushuka kwa thamani ya shilingi.” alisema Dk Kigoda.

Mbunge huyo wa Handeni (CCM), alisema mapendekezo hayo hayajaeleza kwa kina namna sekta ya fedha itakavyosaidia katika kutatua tatizo la uhaba mkubwa wa mitaji unaohitajika kusaidia kukuza uchumi wa Tanzania.

“Hivi sasa tunazo takriban benki 45 na taasisi kadhaa za fedha lakini bado wananchi wengi hawajapata fursa ya kutumia huduma za kifedha katika shughuli zao za kuibua mapato yao na kupata ajira,” alisema.

Katika mapendekezo hayo ya kamati, Dk Kigoda alitaka kutumika kwa sheria mpya ya madini, kampuni za simu zitozwe kodi kama inavyofanyika katika nchi nyingine za Afrika na kodi za majengo.

Alisema mpango huo ulipaswa kujikita katika kuagiza namna ya kudhibiti matumizi mabaya ya fedha katika halmashauri nyingi na ubainishe usimamizi wa fedha na kuagiza ni hatua gani zichukuliwe ili kupunguza matumizi mabaya ya fedha.

Wabunge walichangia mpango huo waliupinga. Mbunge wa Nkasi Kaskazini (CCM), Ally Kessy alisema anapata hofu ya taifa kujikuta likiomba fedha za misaada kutoka nchi ya Cameroon kwa kushindwa kukusanya kodi.

Alishangaa Serikali katika mpango huo kuelezea kuongeza uzalishaji wa matunda wakati haina uwezo wala kuzalisha matunda huku akiponda hoja ya kwamba itaimarisha viwanda wakati yenyewe ndiyo iliyoviua.

Mbunge wa Kilwa Kaskazini (CCM), Murtaza Mangungu, aliishangaa Serikali kujivunia kuwa nchi ina amani na usalama wakati haina usalama kutokana na watu kuwa na njaa... “Hakuna vita mbaya kama taifa kuwa na watu wenye njaa. Tatizo la mfumuko wa bei hasa katika vyakula ni kubwa kutokana na kutokuwepo kwa uthibiti wa bei hizo.”

Akiwasilisha mpango huo, Wassira alitaja baadhi ya maeneo ya kipaumbele kwa mwaka 2012/2013 kuwa ni miundombinu, uzalishaji na usambazaji umeme, barabara, kilimo, viwanda, utalii, huduma za kifedha na tekinolojia ya habari na mawasiliano.

Wassira alisema ili kupunguza pengo katika bajeti ya maendeleo na pia kuchochea kasi ya utekelezaji wa mpango wa mwaka na kutekeleza miradi ya kimkakati, itailazimu Serikali kukopa mikopo maalumu kwa ajili ya kutekeleza miradi hiyo.

Kwa kuanzia katika mwaka wa fedha wa 2012/2013, Serikali itahitaji kukopa Dola za Marekani 540 milioni sawa na Sh864 bilioni mahsusi kwa ajili ya kusaidia uwekezaji wa kimkakati kwa sekta binafsi ili iweze kuwekeza katika miradi ya maendeleo.

Zitto: Sasa tunajipanga

Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe amesema baada ya Pinda kugoma kuwachukulia hatua mawaziri hao, chama chake sasa kinajipanga kufanya mazungumzo na vyama vyote ambavyo wabunge wake walitia saini kukubaliana na hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu huyo ili waone namna ya kuitisha maandamano nchi nzima.

“Lazima Watanzania waelewe suala la kutaka mawaziri hawa wajiuzulu si la Wabunge wa Chadema wala la Zitto, hili ni la wabunge wote isipokuwa UDP na nyinyi ni mashahidi kuwa waliopiga kelele sana ni wabunge wa CCM. Sasa tunafanya mazungumzo na vyama vilivyounga mkono hoja hiyo ili tupange kwa pamoja ni kwa namna gani maandamano hayo yanapaswa kufanywa,” alisema na kuongeza:

“Tunataka kumwambia Rais Kikwete kuwa gharika inakuja na asitafute mchawi ni ama awaondoe mawaziri wanaotuhumiwa kwa ufisadi na utendaji mbovu au wakumbane na Tsunami ya nguvu ya umma.”
HABARI HII KWA HISANI YA GAZETI LA MWANANCHI

Hakimu ambembeleza Lulu mahakamani



 
MSANII wa filamu, Elizabeth Michael Kimemeta maarufu kama Lulu, jana alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu huku akibubujikwa machozi kiasi cha kumfanya Hakimu Ritha Tarimo ambembeleze ili kumnyamazisha. Lulu anashtakiwa mahakamani hapo kwa kutuhuma za kumuua msanii mwenzake, Steven Kanumba na alifikishwa jana kwa mara ya pili akiwa chini ya ulinzi mkali wa askari Magereza na Polisi.

Lulu alifikishwa mahakamani hapo saa 3:06 asubuhi akiwa katika basi dogo la Magereza pamoja na mahabusu wengine wanawake ambalo lilikuwa likisindikizwa na magari mengine mawili na alikuwa chini ya ulinzi wa askari sita wa kike wa Magereza na askari mmoja wa kike wa Polisi wakishirikiana na askari wa kiume wa Magereza zaidi ya sita.

Mara baada kuingia katika chumba cha Mahakama, Lulu ambaye alikuwa amevalia dira jekundu alianza kulia kwa uchungu hali ambayo ilimlazimu Hakimu Tarimo pamoja na baadhi ya askari kumnyamazisha.
Kutokana na kujaa kwa watu mahakamani hapo, askari wa Kikosi Maalumu cha Magereza walilazimika kuufunga mlango wa Mahakama hiyo ili kesi hiyo isikilizwe.

Baada ya kesi hiyo kutajwa, Wakili Mwandamizi wa Serikali Elizabeth Kaganda aliiomba Mahakama iamuru watu wote watoke nje kwa sababu walikuwa wamefunga njia ili mtuhumiwa huyo aweze kupitishwa.

Hakimu Tarimo alikubaliana na ombi hilo na kuwaamuru askari kusafisha njia ili waweze kumpitisha msanii huyo kwa kile alichosema kuwa Lulu bado ni mtuhumiwa na anaweza kuumizwa.
“Askari safisheni njia ili mtuhumiwa aweze kupita kwa sababu yeye bado ni mtuhumiwa anaweza kuumizwa,"alisema Hakimu Tarimo.

Baada ya kutolewa kwa amri hiyo, askari walitimiza wajibu wao na muda mfupi njia ilipatikana na msanii huyo kutolewa mahakamani hapo.

Jopo la mawakili
Katika kesi hiyo, Lulu anatetewa na jopo hilo la mawakili akiwemo Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (CHRAGG), Joaquine De- Melo, Kenedy Fungamtama, Peter Kibatala na Fulgence Massawe.

De- Melo  pia aliwahi kuwa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanzania (TLS) na mshindi wa Tuzo ya Mwanamke Jasiri Tanzania ya Martin Luther King.

Fungamtama ambaye ndiye kiongozi wa jopo la mawakili hao wanaomtetea Lulu, anakumbukwa kwa kuitetea kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans, katika kesi dhidi ya Tanesco, ambayo alishinda na shirika hilo kuamriwa kuilipa kampuni hiyo  zaidi ya Sh94 bilioni kwa kuvunja mkataba.
Kibatala ambaye pia anamtetea kada wa Chadema, Fred Mpendazoe katika kesi ya uchaguzi Jimbo la Segerea, pia ni Makamu wa Rais wa TLS, wakati Massawe anatoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC).

Mawakili hao walijitokeza jana mbele ya Hakimu Tarimo tayari kumtetea Lulu na baada ya mawakili hao kujitambulisha, Wakili Kaganda alisema upelelezi wa kesi bado haujakamilika na kuiomba Mahakama iipangie tarehe nyingine.

Hakimu Tarimo aliiahirisha kesi hiyo hadi Mei 7, mwaka huu itakapofikishwa mbele ya Mahakama hiyo kwa ajili ya kutajwa.

Kwa mara ya kwanza Lulu alifikishwa mahakamani hapo Aprili 10, mwaka huu mbele ya Hakimu Mkazi, Augustina Mmbando  akikabiliwa na la shtaka hilo la mauaji.

 Wakili Kaganda alimsomea hati ya mashtaka alidai kuwa Aprili 7, mwaka huu katika maeneo ya Sinza Vatican, Wilaya ya Kinondoni, mtuhumiwa alimuua  Kanumba. Kanumba alifariki dunia siku hiyo saa 9:00 usiku kwa kile kilichodaiwa kuwa ni baada ya ugomvi baina yake na Lulu. HABARI KWA HISANI YA MWANANCHI COMMUNICATION
  

Monday, April 23, 2012

Picha Za Elizabeth Michael ' Lulu' Alipotinga Mahakama Ya Hakimu Mkazi Kisutu Leo,Kesi Kusikilizwa tena Mei 7


Mshatkiwa Elizabeth Michael |(17), ' Lulu'  akielekea kupanda ngazi na kupandishwa Kizimbani Kesi hiyo  ilikuja kwa ajili ya kutajwa  Upelelezi haujakamilika hiyo ni kwa mujibu wa Wakili wa Serikali Elizabeth Kaganda alisema mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Rita Tarimo  hivyo kesi hiyo  itatajwa tena Mei 7 mwaka huu. Mtuhumiwa amerudishwa rumande.
 Akizindikizwa ndani ya chumba cha Mahakama ya hakimu mkazi kisutu jijini Dar es Salaam leo
Mshtakiwa akipanda ngazi kuelekea Kizimbani ambalo kesi yake ilitajwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es Salaam huku akiwa katika ulinzi mkali kutoka kwa askari  Magereza.Picha na Mdau Khadija Kalili
KWA HISANI YA HAKI-NGOWI

Wanajeshi 400 wa Sudan Kusini waripotiwa kuuwawa katika mapigano.

Mzozo juu ya Heglig na vinu vyake vya mafuta vyenye utajiri umepelekea wasi wasi wa vita kamili.
Eneo lililoshambuliwa na bomu na majeshi ya anga ya Sudan huko Sudan Kusini.
Picha AP
Eneo lililoshambuliwa na bomu na majeshi ya anga ya Sudan huko Sudan Kusini.
 
Maafisa wa Sudan  wanajeshi  400 wa Sudan Kusini waliuwawa wakati wa mapigano katika mzozo wa mji  wa Heglig, eneo la kuzalisha mafuta linalodaiwa na nchi zote mbili.
Majeshi ya Sudan Kusini yamekamilisha uondokaji wao Heglig jumapili, wakisema idadi ya askari waliouwawa ni ndogo na  kile Sudan wanachodai. Idadi  ya waliojeruhiwa Sudan ni haiwezekani  kuthibitisha.
Mzozo juu ya  Heglig na vinu  vyake  vya mafuta vyenye utajiri umepelekea  wasi wasi wa vita kamili ikiwa ni chini ya mwaka mmoja baada  ya Sudan kusini kujitangazaia uhuru wake kutoka kaskazini.

Sudan yashambulia kusini


Uharibu uliotokea kwenye kisima cha mafuta kwenye jimbo la Unity, Sudan Kusini
Juma lilopita, wanajeshi wa Sudan Kusini waliteka visima muhimu vya mafuta vya Sudan kaskazini, huko Heglig, na kuzusha malalamiko ya kimataifa na msukosuko mkubwa.
Na picha za satalaiti ya Marekani zinaonesha kuwa sehemu muhimu ya miundo mbinu kwenye visima hivo iliharibiwa vibaya.
Siku ya Ijumaa Wasudan Kusini waliondoka, au walitimuliwa kwa mujibu wa taarifa za Sudan.
Na huko kusini, miripuko kadha kwa mpigo ilisikika masafa ya maili kadha.
Sudan Kusini ilisema hilo lilikuwa jaribio la kuharibu mtambo wa kusafisha mafuta katika kisima cha mafuta kwenye jimbo la Unity.
Naibu wa mkuu wa idara ya usalama ya jeshi la Sudan Kusini, Jenerali Mac Paul, alisema kulitokea mapambano kidogo baina ya wanajeshi wake na wale wa Kaskazini, karibu na mpaka wenye utatanishi.
Haikuwezekana kupata taarifa ya jeshi la Sudan.
Lakini ni wazi kuwa Sudan Kusini ina wasiwasi kuwa itashambuliwa na Sudan.
Juma hili Rais Omar el Bashir amesema anataka "kuikomboa" Sudan Kusini kutoka "wadudu" wanaoingoza nchi hiyo.
Alikasirika baada ya Sudan Kusini kuviteka na kuvikalia kwa juma zima visima vya mafuta vya Heglig, chanzo cha pato kubwa kwa serikali ya Khartoum.
Makamo wa rais wa Sudan Kusini, Riek Machar, aliiambia BBC kwamba wanajeshi wake wako tayari kuiteka tena Heglig, iwapo watashambuliwa tena.

Sarkorzy ashindwa kwenye uchaguzi

Mgombea urais kwa tiketi ya chama cha kisoshalisti nchini Ufaransa Francois Hollande, ameshinda duru ya kwanza ya uchaguzi nchini humo.
Kura nyingi zikiwa zimehesabiwa Bw Hollande tayari amepata asilimia 28 ya kura.
Francois Hollande
Kiongozi huyo anasema wafaransa wanaimani naye
 
 Nicolas Sarkozy anafuatia kwa asilimia 27 hii ikiwa ni idadi ndogo zaidi kwa rais yoyote wa taifa hilo ambaye amewahi kugombea tena kiti hicho.
Haijawahi kutokea kuwa rais aliyemadarakani anashindwa kwenye duru ya kwanza ya uchaguzi.
Na matokeo haya yanampa mpinzani wa Rais Sarkorzy, Francois Hollande nafasi nzuri sana katika duru ya pili ya uchaguzi huo utakaofanyika baada ya wiki mbili.
Hata hivyo kilicho washangaza wengi baada ya matokeo hayo kutangazwa ni idadi ya kura chama kinacho egemea upande wa kulia kilipata.
Kwa makadirio tu, mtu mmoja kati ya wapiga kura watano nchini Ufaransa alikipigia kura chama hicho, hii ikiwa idadi kubwa zaidi ya kura chama hicho cha Front Nationale kilicho pata kwenye uchaguzi wowote nchini humo.
Rais Sarkorzy anasema matokeo hayo yanaonyesha hali ya wasi wasi raia wa nchi hiyo wanayo na ni kura ya maoni dhidi ya utawala wake.
Hata hivyo ametoa changamoto kwa mpinzani wake ajitokeze kwenye mdahalo kati yao kabla duru ya pili ya uchaguzi huo.
Lakini bila shaka kutokana na uchache wa kura alizopata dhidi ya Rais Sarkorzy, kiongozi huyo wa chama cha kisoshalisti, Francoise Hollande atakuwa makini sana asipoteze kura muhimu.
Bw Hollande anasema wafaransa wanaimani na mradi wake kwa nchi hiyo ambao umelenga kurejesha haki, usimamizi bora wa uchumi wa nchi, ukuzaji wa nafasi za kazi, kulinda viwanda na kujiandaa vyema kwa siku za usoni.
  BBC SWAHILI.COM

Sunday, April 22, 2012

*WAWILI WAGOMA KUWASILISHA BARUA , PINDA KUTOA TAMKO KESHO



Na Waandishi Wetu,Dodoma
WAKATI kishindo cha shinikizo la kutakiwa kujiuzulu mawaziri nane wa Serikali ya Rais Jakaya Kikwete kikizidi kurindima, Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema Serikali itatoa tamko lake rasmi kesho.

Awali Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenister Mhagama aliwaambia waandishi wa habari juzi usiku kuwa chama hicho kimefanya maamuzi magumu ambayo yangetangazwa na Pinda mjini hapa jana.

Hata hivyo, Waziri Mkuu Pinda alipoombwa na waandishi wa habari jana kuzungumzia sakata hilo, hakukanusha wala kukiri kuwapo kwa azimio hilo zaidi ya kusema wananchi wasubiri hadi kesho atakapotoa taarifa rasmi.
Alipoulizwa kama kuna mawaziri ambao wameshawasilisha barua zao za kujiuzulu hadi kufikia jana mchana, Pinda alijibu kwa kifupi kuwa ‘bado hatujapokea, lakini kama wapo watatuletea tu”.
Ingawa Waziri Mkuu hakukiri kupokea barua yoyote, taarifa zisizo rasmi, zilisema mawaziri watano waliokumbwa na msukosuko huo wamekabidhi barua zao huku Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Cyril Chami akikataa kufanya hivyo.

Mwingine ambaye anatajwa kuwa hajawasilisha barua yake, ni Waziri wa Fedha Mustapha Mkulo ambaye kwa sasa yuko nje ya nchi.
Chami ajitetea

Dk. Cyril Chami amesema hataandika barua ya kujiuzulu wadhifa huo na kusema anawaachia wananchi wapime kama kweli anastahili kujiuzulu ama la.
Akizungumza na Mwananchi Jumapili jana alisema yuko tayari kujiuzulu endapo tu wananchi na wabunge  watampa fursa ya kusikiliza utetezi wake na kama bado wataona ana makosa,yuko tayari kuachia ngazi.
Dk Chami ni mmoja wa mawaziri ambao Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupitia kikao cha Wabunge wa chama hicho, kimewapa muda hadi kufikia kesho wawe wameandika barua za kujiuzulu.
Kiini cha D. Chami kutakiwa kujiuzulu, ni kauli za Wabunge wa CCM kuwa anamkingia kifua Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango nchini (TBS), Charles Ekelege anayetuhumiwa kwa ufisadi.
Hata hivyo Dk Chami alisema hadi jana wizara yake ilikuwa haijapatiwa ripoti ya Mamati Maalumu ya Bunge ya Mashirika ya umma iliyokwenda kumchunguza Ekelege katika nchi za Hongkong na Singapore.
“Nataka wananchi wanielewe nitamwajibishaje Ekelege wakati ripoti ya kamati teule ya Bunge iliyomchunguza mimi sina…ningejengaje hoja kwa Rais bila kuwa na tuhuma zake?”alihoji D. Chami.
Alisema Mkurugenzi wa TBS ni mteule wa Rais na kuna taratibu zake ambapo taarifa ya kamati hiyo ndiyo ingeisadia Bodi ya Wakurugenzi ya TBS kumjadili na kupitisha maamuzi,”alisema.
Alifafanua hata ripoti maalumu ya ukaguzi iliyofanywa na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) hawakuwa wamepewa na wamepatiwa siku tatu zilizopita mjini Dodoma.
“Bado najiuliza CAG alikuwa na agenda gani na wizara yangu kwa sababu hakutupa ripoti yake lakini akawapa baadhi ya wabunge mpaka tulipofuatulia juzi baada ya kelele za wabunge”alisema.
Aliongeza kusema Waziri wa Fedha, Mustapha Mkulo, leo anashutumiwa kwa kumsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Shirika Hodhi la Mashirika ya Umma(CHC) bila kufuata utaratibu.
“Utashangaa leo Mkulo anashutumiwa kwa kutofuata taratibu kumsimamisha Mkurugenzi Mkuu wa CHC lakini leo mimi nashinikizwa nimsimamishe kazi Mkurugenzi wa TBS bila kufuata taratibu,”alisema.
Dk Chami alisema amejitahidi kuomba taarifa hiyo ya Kamati Teule iliyomchunguza Ekelege lakini hadi jana hajapatiwa zaidi ya kuambiwa ilipelekwa kwa Spika na hajaambiwa baada ya hapo ilikwenda wapi.
Hata hivyo habari za uhakika ambazo gazeti hili inazo , zinaonyesha kuwa baada ya ripoti hiyo ya kamati kufika kwa Spika, Spika naye aliipeleka kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Katika kuthibitisha Wizara ya Viwanda na Biashara haikuwa imeipata barua hiyo, Februari 2,2012 Katibu Mkuu, Joyce Mapunjo alimwandikia barua Katibu wa Bunge akimkumbusha awapatie ripoti hiyo.
Barua hiyo yenye kumbukumbu namba GA96/352/01 iliyopelekwa kwa Katibu wa Bunge Dk Thomas Kashilila, ilisema”nimeona nikukumbushe unisaidie ripoti hiyo niweze kutekeleza maagizo ya kamati”.
Kwa mujibu wa uchunguzi huo, Februari 10,2012 Kamati za PAC na POAC na ile ya Viwanda na Biashara zilikutana Dodoma ambapo Kamati iliendelea kumtuhumu Mtendaji Mkuu wa TBS.
Katika kikao hicho, wizara iliagizwa kuwasilisha kwa CAG ripoti ya idadi ya magari yaliyokaguliwa na mapato yake, na wizara ikakabidhi ripoti hizo  Februari 15,2012 kwa barua yenye kumb GA.96/352/01.
Ni kwa maelezo hayo, Dk. Chami alidai tangu wakati huo ofisi yake haijawahi kupokea ripoti nyingine yoyote iwe ya CAG au kutoka kwa Spika zaidi ya kufahamu kuwapo kwake bungeni wiki hii.
Dk Chami alifafanua kuwa kukosekana kwa ripoti hizo kulimfanya afungwe mikono ya kwenda kwa Rais kumshauri amuondoe Ekelege kwa kuwa hakuwa na ripoti iliyokuwa ikionyesha tuhuma zake.
Kutokana na msingi huo, Dk. Chami alisema chombo alichobakia nacho kuchukua maamuzi ni Bodi ya Wakurugenzi ya TBS na bodi hiyo iliundwa na kuzinduliwa Machi 29, 2012.
Dk Chami alisema bodi hiyo ilikutana Aprili 5,2012 na Wizara yake ikapokea ushauri wa Bodi hiyo Machi 19,2012 na wakati ripoti ya ukaguzi maalumu wa CAG akiipokea Aprili 18 akiwa Bungeni Dodoma.

 


Omari Nundu
Kwa upande wake Waziri wa Uchukuzi,Omari Nundu jana alitumia Bunge kurusha kombora kwa Kamati ya Mindombinu kuwa imekuwa na taarifa zisizo sahihi.
Nundu alisema taarifa zote juu yake ni za uongo huku akikanusha kwamba hajawahi kusaini makubaliano (MoU) yoyote kuhusu mradi wa upanuzi wa Bandari ya Dar es Salaam gati  namba 13 na 14.

Ngeleja
Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja ambaye pia ni Mbunge wa Sengerema, alipoulizwa na mwandishi wetu kupitia ujumbe mfupi wa maandishi(SMS) alijibu kwa kifupi ‘Tuziachie mamlaka za maamuzi”.
Mawaziri wanaotakiwa kujiuzulu ili kuinusuru Serikali ni Waziri wa Fedha, Mustapha Mkulo,Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja na Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige.
Wengine ni Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Profesa Jumanne Maghembe, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hadji Mponda na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Lazaro Nyalandu.
Taarifa zilizopatikana juzi usiku zilieleza kuwa katika kikao hicho, mawaziri hao kwa pamoja waliwekwa katika eneo maalumu na wakawa wakiitwa mmoja mmoja kwa ajili ya mahojiano na wabunge na baadaye kupewa msimamo wa chama.
Baada ya kumalizika kwa kikao hicho, Waziri Mkuu akaendesha kikao kingine cha faragha, safari hii kikimhusisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali,Frederick Werema na Waziri William Lukuvi.

Wengine walioitwa katika kikao hicho ni Katibu wa Uchumi na Fedha wa CCM, Mwigulu Mchemba,Katibu wa Oganaizesheni na Mahusiano ya Nje Januari Makamba na Katibu wa wabunge wa chama hicho, Jenister Mhagama.

Hata hivyo mwenye mamlaka ya kuwafukuza Mawaziri kwa mujibu wa Katiba ni Rais Jakaya Kikwete aliyewateua ingawa hata hivyo badhi ya wabunge wanamtuhumu Rais kuwa si mtu wa kufanya maamuzi haraka na kwa shinikizo.

Jana baadhi ya mawaziri wanaotakiwa kuachia ngazi waliingia katika ukumbi wa Bunge na kukalia viti vyao lakini mara baada ya kuahirishwa kwa kikao, waliondoka haraka katika viwanja vya Bunge.

Baadhi yao walipotafutwa  kwa simu ili watoe ufafanuzi na msimamo wao kuhusiana na azimio hilo la CCM, ama simu zao zilikuwa hazipatikani kabisa na zingine hazikupokelewa, zilikatwa.

Zitto aendelea kutafuta saini

Katika hatua nyingine,Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe alisema hoja ya kumpigia Waziri Mkuu kura ya kutokuwa na imani ipo pale pale kama mawaziri wanaotajwa kwa ufisadi hawatajiuzulu kufikia kesho.
“Sisi tunasema bila kumwajibisha Waziri Mkuu hawa mawaziri waliotajwa hawatatoka na wasipotoka madudu haya yatarudia…kwa hiyo ni wao mawaziri kupima na kuwajibika au wamweke reheni Waziri Mkuu,”alisema.
Mbunge huyo alirejea wito wake wa kuwaomba wabunge wenye uchungu na ubadhirifu na ufisadi waunge mkono utiaji wa saini hizo na kwamba kama mawaziri watajiuzulu ifikapo Jumatatu, wataondoa hoja hiyo.
Kwa upande wake, Kiongozi wa Kambi rasmi ya upizania Bungeni, Freeman Mbowe alirejea msimamo wake wa kuomba kufanyiwa mabadiliko ya katiba ya nchi na kanuni za Bunge ili Spika asiwe anatokana na chama chochote cha siasa.
Mbowe alitoa kauli hiyo kutokana na kile alichodai,  hatua ya Spika Anne Makinda kutafsiri vibaya kanuni za Bunge na Katiba ya nchi ili tu kuilinda Serikali na Waziri Mkuu wake ili asipigiwe kura ya kutokuwa na imani.
“Mambo ya ajabu sana eti Spika anasema hili zoezi letu ni batili…sisi tunamshangaa, wanasheria wanamshangaa na hata wananchi wanamshangaa… anatoleaje mwongozo kwa kitu ambacho hakipo mezani kwake?”alihoji.
Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai, alisema kanuni inataka ili hoja ya kumpigia kura ya kutokuwa na imani na Waziri mkuu iweze kufikishwa ofisi ya Spika, ni lazima ipate sahihi za wabunge 70 na ndicho wanachokifanya.

Wasomi wazungumza

Baadhi ya wasomi wa Chuo Kikuu wamelitaka Bunge kufuata sheria na kanuni za Bunge kabla ya kufanya maamuzi hayo kwa sababu mawaziri hao wanaripoti kwa Rais Jakaya Kikwete na si Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam jana, wasomi hao walisema kuwa, kutokana na hali hiyo wabunge hao wanapaswa kufuata kanuni ili waweze kutambua kuwa mwenye mamlaka ya kuwaondoa mawaziri hao ni  Rais na si Waziri Mkuu, hivyo basi kumlazimisha aondoke madarakani ni sawa na kumuonea.

“Mimi naona wanamuonea bure Waziri Mkuu Pinda, kwa sababu hana mamlaka ya kuwaondoa Mawaziri madarakani badala yake wanatakiwa kuangalia kanuni kwanza ndipo waweze kufanya maamuzi,”alisema Profesa Simon Mbilinyi mwasiasa mstaafu nchini.

Aliongeza kutokana  na hali hiyo wabunge hao walipaswa kumuandikia barua Rais Kikwete na kumtaarifu kuwa mawaziri wake wameshindwa kufanya kazi badala yake wanatakiwa kuwajibika kulingana na makosa waliyofanya.

Alisema kutokana na hali hiyo maamuzi ambayo yangeweza kutolewa na rais yangekuwa sahihi kwa sababu yamefuata sheria na taratibu zilizotungwa na Bunge.

Alisema kitendo cha wabunge hao kumshinikiza Waziri Mkuu kujiuzulu au kuwaondoa mawaziri hao ni kinyume na sheria na ni sawa na kumuonea, jambo ambalo linaweza kumfanya afanye maamuzi bila ya kufuata taratibu.

Hata hivyo, Profesa Abdalah Safari alisema kuwa wabunge wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) ni wanafiki, na kwamba wanashindwa kufanya maamuzi mpaka wasubiri nguvu kutoka kwa wapinzani.

Alisema kutokana na hali hiyo wabunge hao wamepoteza mwelekeo na kwamba wamejaa woga jambo ambalo limesababisha kuendekeza ufujaji wa mali za umma kwa makusudi.

Naye Makamu Mkuu Chuo Kikuu cha Matakatifu Agustino cha Mwanza (Sauti) Dk  Charles Kitima amesema  mchakato unaofanywa na wabunge kwa   lengo la kumg’oa Waziri Mkuu Pinda sio suluhu ya kutibu tatizo la uwajibikaji kwa viongozi  serikalini.

 “Tunalia watu wajiuzulu wakati tumebaki na mfumo ambao unaruhusu siasa chafu, Mahakama inaingiliwa katika maamuzi yake Tume ya Uchaguzi haiko huru, hili haliwezi kuleta mabadiliko sababu Rais atateua mtu mwingine kufanya kazi hiyo na shughuli zitaendelea kama kawaida”alisema Dk Kitima.

Dk Kitima ambaye alikuwa akichangia  mada  katika kipindi cha jicho letu katika habari kinachorushwa na kituo cha Televisioni cha Star Tv cha jijini Mwanza jana, alisema njia pekee ambayo inaweza kuleta  mabadiliko ni kubadilisha mfumo utakaowezesha viongozi kuwajibika kwa wananchi.

“Walijiuzulu Edward Lowasa, Nazir Karamagi na Dk Ibrahim Msabaha nini kimebadilika, rais ameteua wengine matatizo bado yanaendelea serikalini tatizo si watu bali mfumo uliopo ambao unatoa fursa kwa viongozi na watendaji kuwajibika kwa waliowateua”alisema Dk Kitima.

Habari hii imeandikwa na Daniel Mjema na Habel Chidawali, Dodoma, Patricia Kimelemeta, Geofrye Nyang’oro

Orodha ya wabunge waliosaini:
      
  1. 2.     Rashid Ali Abdallah – CUF
  2. 3.    Chiku Aflah Abwao- Chadema
  3. 4.     Saluim Ali Mbarouk – CUF
  4. 5.    Salum Khalfam Barwany –  CUF
  5. 6.     Deo Haule  Filikuchombe- CCM
  6. 7.    Pauline Philipo Gekul- Chadema
  7. 8.    Asaa Othman  Hamad- CUF
  8. 9.     Prof.Kuliyokela Kahigi- Chadema
  9. 10.    Naomi  Mwakyoma Kaihula – Chadema
  10. 11.     Sylvester Kasulumbayi- Chadema
  11. 12.     Raya Ibrahim Khamis  - Chadema
  12. 13.     Mkiwa Hamad Kiwanga  -  CUF
  13. 14.     Susan  Limbweni Kiwanga- Chadema
  14. 15.     Grace Sindato Kiwelu –Chadema
  15. 16.     Kombo Khamis Kombo – cuf
  16. 17.     Joshua  Samwel  Nassari – Chadema
  17. 18.     Tundu Antiphas Lissu- Chadema
  18. 19.     Aphaxar  Kangi Lugola- CCM
  19. 20.    Susan Anselim Lymo- Chadema
  20. 21.     Moses Machali – NCCR Mageuzi
  21. 22.     John Shibuda Magalle – Chadema
  22. 23.    Faki  Haji  Makame-  CUF
  23. 24.     Esther Nicholas Matiko- Chadema
  24. 25.     Joseph Osmund Mbilinyi- Chadema
  25. 26.    Freman  Aikaeli Mbowe- Chadema
  26. 27.    Kurudhum Jumanne Mchuchuli – Chadema
  27. 28.     Halima James Mdee-Chadema
  28. 29.    John John Mnyika- Chadema
  29. 30.     Augustino Lyatonga Mrema- TLP
  30. 31.     Maryam Salum  Msabaha- Chadema
  31. 32.     Peter Msingwa-chadema
  32. 33.    Christowaja Gerson Mtinda- Chadema
  33. 34.     Philipa Geofrey Mturano- Chadema
  34. 35.    Christina Lissu Mughwai- Chadema
  35. 36.    Joyce John  Mukya – Chadema
  36. 37.    Mchungaji  Israel  Yohane  Natse – Chadema
  37. 38.    Philemon Ndesamburo- Chadema
  38. 39.     Ahmed  Juma Ngwali-  CUF
  39. 40.    Vincent  Josephat  Nyerere- Chadema
  40. 41.     Rashid  Ali Omar-  CUF
  41. 42.    Meshack  Jeremiah Opulukwa- Chadema
  42. 43.     Lucy Philemon Owenya- Chadema
  43. 44.     Rachel Mashishanga- Chadema
  44. 45.     Mhonga Said Ruhwanya – Chadema
  45. 46.     Conchesta Rwamlaza – Chadema
  46. 47.    Moza Abedi  Saidy-  CUF
  47. 48.    Joseph  Roman Selasini – Chadema
  48. 49.     David Ernest  Silinde- Chadema
  49. 50.     Rose Kamili Sukum  - Chadema
  50. 51.     Cecilia Daniel Paresso- chadema
  51. 52.    Kabwe Zuberi Zitto- Kigoma Kaskazini
  52. 53.     Magdalena Sakaya –  CUF
  53. 54.     Rebecca Mngodo-  CUF
  54. 55.     Sabreena Sungura -Chadema
  55. 56.    Hamad Rashid Mohammed- CUF
  56. 57.    Rukia Kassim Ahmed- CUF
  57. 58.    Mustapha Boay Akoonay -Chadema
  58. 59.     Abdalla Haji Ali -CUF
  59. 60.    Khatibu Said Ali -CUF
  60. 61.     Hamad Ali Hamad -CUF
  61. 62.      Riziki Omar Juma -CUF
  62. 63.     Haji Khatibu  Kai -CUF
  63. 64.     Anna Marystella John Malack -Chadema
  64. 65.     Hamad Rashid Mohamed  -CUF
  65. 66.     Rajab Mbarouk Mohamed -CUF
  66. 67.     Thuwayba Idrissa Muhamed -CUF
  67. 68.      Masoud Abdallah Salum -CUF
  68. 69.     Muhamad Ibrahim Sanya -CUF
  69. 70.     Ali Khamis Seif -CUF
  70. 71.     Haroub Muhammed Shamis -CUF
  71. 72.     Amina Amour Nassoro -CUF

Jahazi la CCM lazidi kuzama



UPEPO wa wanachama wa CCM kujiunga na Chadema umezidi kushika kasi baada ya viongozi zaidi wa chama hicho na mamia wanachama kuhamia Chadema.  Viongozi wa CCM waliohamia Chadema  ni Wilaya ya Monduli, Wilaya za Sengerema, na Kikundi cha Kwaya cha Uhamasishaji wa chama hicho Wilaya ya Magu na mamia ya wachama kutoka katika maeneo hayo.
Akizungumza na Mwananchi Jumapili kwa njia ya simu jana, Mwenyekiti wa Chadema, Wilaya ya Monduli, Amani Ole Selenga amesema chama chake kimepokea jumla ya wanachama 300 wa CCM katika kata mbili za Makuyuni na Mto wa mbu wilayani Monduli.

Aliongeza kuwa wengi wa wanachama hao ni wajumbe wa serikali za vijiji na wajumbe wa nyumba kumi.
Kwa mujibu wa Ole Selenga, taarifa za wanachama hao kukimbilia Chadema zilimshtua Mbunge wa Monduli na Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa na kudai kuwa mbunge huyo alipanga kurejea jimboni kuzima moto huo.
Mkoa wa Mwanza Katika hatua nyingine zaidi ya wanachama 95 wa CCM kutoka Wilaya za Magu na Sengerema wamerudisha kadi za CCM na kujiunga na Chadema jana.
Wanachama hao ambao kati yao, 45 ni wanakwaya maarufu ya uhamasishaji ya Ngómbe ya Magu ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikitumiwa katika kampeni kuhamasisha wananchi kuchagua CCM.
Akitangaza kujiunga wanakwaya hao, Katibu wa Chadema Magu, Bahati Simon alisema jana kuwa wamechukua uamuzi huo baada ya kuona CCM haijawaletea maendeleo wananchi wala wao wenyewe.
Katika mkutano wa hadhara uliofanyika jana mjini Sengerema na kuhutubiwa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbrod Slaa, wanachama 50 wa CCM walihama na kujiunga na Chadema.
Katika mkutano huo, diwani wa CCM Kata ya Lugata kutoka Wilaya ya Sengerema Adrian Tizeba, alitangaza kujiunga na Chadema.  Diwani huyo ambaye ni ndugu wa Mbunge wa Buchosa (CCM), Dk Charles Tizeba, alisema ameamua kuhamia Chadema kwa hiari yake mwenyewe  Diwani mwingine aliyehama CCM na kuingia Chadema ni Hamis Mwagao wa Kata ya Nyampulukano ambaye pia  Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya UVCCM, Wilaya ya Sengerema John Tungu.   Viongozi CCM Arusha waita Dar
Wakati hali ikiendelea kuwa tete, ndani ya CCM viongozi wa ngazi ya juu wa CCM Mkoa wa Arusha wameitwa makao makuu ya chama jijini Dar kueleza kinachoendelea mkoani humo.   Habari za uhakika kutoka ndani ya viongozi wa CCM, zimeeleza kuwa Katibu wa UVCCM Mkoa wa Arusha, Abdalah Mpokwa na Katibu wa Itikadi mkoani humo, Loota Sanare  Jumatano wiki hii, waliitwa ghafla makao makuu ya CCM na walitarajia kurejea jana jioni kwa ndege.  “Ni kweli kuna viongozi wameitwa haraka Dar es Salaam nadhani wametakiwa  ili kueleza kinachotokea Arusha,” alisema Kiongozi mmoja wa CCM ambaye jina lake linahifadhiwa.  Wakati viongozi hao wakiwa wameitwa Dar es Salaam, viongozi wengine wa CCM wa ngazi ya mkoa na wilaya, kuanzia juzi walikuwa katika wilaya za Ngorongoro katika kata za Enduleni, Longido na Monduli kufuatilia taarifa za viongozi na wanachama wao kuhamia Chadema.  Katibu wa Uenezi na Itikadi wa CCM, Mkoa wa Arusha, Sanare alikiri jana kuwa alikwenda jijini Dar es Salaam ghafla muda mfupi baada ya kurejea safari yake binafsi Nairobi, Kenya. Hata hivyo alikanusha kuitwa na viongozi wa juu wa CCM.  “Ni kweli nipo Dar es Salaam, lakini sipo kwa mambo ya CCM nina mambo yangu, haya mambo ya kuhama watu ni haki yao ila vyombo vya habari mnayakuza sana,” alisema Sanare.   Diwani wa CCM Kata ya Endeleni, James Moringe alikiri kwenda katika Kata hiyo, lakini alikanusha taarifa za kuhama kwa viongozi wa CCM wa kata hiyo na kujiunga na Chadema.  “Wapo viongozi huko, lakini wengi wa hawa wanaodaiwa kuhamia Chadema sio viongozi wa CCM na kuhama kwao kunatokana na mgogoro katika moja ya vijiji katika kata hiyo,” alisema Moringe.  Katika Wilaya za Monduli na Longido pia, viongozi wa chama hicho, wamekuwa wakihaha na kukutana na baadhi ya viongozi wakiwasihi kutokihama chama hicho.  “Tunasumbuliwa sana na taarifa za kuondoka mimi nimeamua kurudi kwanza kijijini kutulia kwani sasa hivi ni sawa na vitisho, lakini kuondoka kupo palepale wakati ukifika,” alisema kiongozi mmoja wa UVCCM wilaya ya Monduli.   Naye Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Monduli, Julias Kalanga ambaye jana alitangaza angekutana na wanahabari pamoja na viongozi na wana CCM wengine kutoa msimamo wao,  hakupatikana na muda wote simu zake za mkononi zilikuwa zimefungwa.  Taarifa ambazo Mwananchi Jumapili inazo ni kwamba Kalanga amekuwa akibembelezwa na viongozi wa juu wa CCM kutotangaza kukihama chama hicho, wakati madai yao UVCCM Mkoa wa Arusha yakifanyia kazi.  Mmoja wa viongozi wa CCM katika wilaya hiyo, alisema kutojitokeza jana kutangaza kukihama chama hicho, kunatokana na kutafakari maombi ya kutofanya hivyo pamoja na hali ya kisiasa nchini ilivyo sasa.  “Watu wote wanafuatilia bunge kujua hatma ya Serikali ya CCM na hasa kutimuliwa kwa mawaziri  sasa tumeona tusubiri kidogo kitakachotokea Dodoma ila msimamo wetu upo palepale,” alisema kiongozi mwingine wa CCM.  Dk Slaa
Akihutubia mkutano wa hadhara mkoani Mwanza, Dk Slaa aliwashukia wabunge wa CCM wanaodai ni wapambanaji wa ufisadi kuwa hawana nia ya dhati kwa vile  wanaogopa wimbi la wanachama kukihama chama chao.  Dk Slaa alisema kama kweli wabunge hao wanaojipambanua kama wapambanaji na ufisadi wangekuwa wangejiunga na Chadema tangu mwaka 2007.
 Dk Slaa alisema chama chake kitafungua kesi wiki ijayo kuishtaki Serikali mahakamani kwa makosa ya uvunjaji wa haki za msingi za binadamu.  Akizungumza jana katika mkutano wa hadhara wa Uwanja wa Magereza, Dk Slaa alisema chama hicho kimeamua kufanya hivyo ili kukomesha unyanyasaji na kuwataka wananchi na viongozi wote ambao wamekuwa wakibambikiwa kesi kukusanya taarifa zote ambazo zitakuwa sehemu ya ushahidi wa mashtaka hayo ili mchakato huo ukamilike.  Imeandikwa na Claud Mshana, Frederick Katulanda, Geita, Mussa Juma, Peter Saramba, Arusha

Salva Kiir awaondoa wanajeshi Heglig

Wanajeshi wa Sudan Kusini
Rais wa Sudan Kusini, Salva Kiir ameamrisha wanajeshi wake kuondoka kwenye visima vya Heglig katika mpaka unaozozaniwa kati yake na Jamuhuri ya Sudan.
Wanajeshi wa Sudan Kusini waliteka eneo la Heglig wiki jana ambapo walilaumu utawala wa Khartoum kutumia mahala hapo kama ngome ya kufanya mashambulio.

Awali Hapo Alhamisi Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki moon alitaja kuwepo kwa wanajeshi wa Sudan Kusin kama kinyume na sheria ya kimataifa.
Hata hivyo Umoja wa Mataifa ulitaka Jamuhuri ya Sudan kusimamisha mashambulio dhidi ya Sudan Kusini .
Makabiliano kati ya pande zote yalitishia kuzuka kwa vita vingine. Sudan Kusini ilijiondoa kwa Jamuhuri ya Sudan mwaka jana kufuatia muafaka wa amani ulioafikiwa mwaka 2005 baada ya vita vya zaidi ya miongo miwili.
Hapo Alhamisi, Sudan Kusini ilitoa taarifa na kusema haikuwa na haja ya vita na jirani yake na kusisitiza ingewaondoa wanajeshi wake kutoka Heglig pale Umoja wa Mataifa utatuma waangalizi wake.
Awali rais wa Sudan Omar al-Bashir alitishia kuizima serikali ya Sudan Kusini baada ya kupoteza eneo la Heglig ambalo huzalisha zaidi ya nusu ya mafuta ya Sudan.
Chini ya sheria za kimataifa, Heglig ni sehemu ya Jamuhuri ya Sudan japo mipaka kamili ingali kutambuliwa rasmi.

France votes in first round of presidential poll

 

Francois Hollande (left) and Nicolas Sarkozy Francois Hollande (left) is mounting a strong challenge against President Sarkozy
Polls have opened in France's presidential election, taking place amid widespread concern over the eurozone crisis and high unemployment.
Centre-right incumbent Nicolas Sarkozy is seeking re-election, saying only he can preserve a "strong France".
But he is facing a tough challenge from Socialist Francois Hollande, who has said it is "the left's turn to govern".
There are 10 candidates in all, and if none wins more than 50% of the votes there will be a run-off round on 6 May.
Polls in mainland France and Corsica are open until 18:00 (16:00 GMT), with voting stations in big cities remaining open for a further two hours.
The first official results will be released after the last stations close at 20:00 (18:00 GMT).
President Sarkozy, who has been in office since 2007, has promised to reduce France's large budget deficit and to tax people who leave the country for tax reasons.
He has also called for a "Buy European Act" for public contracts, and threatened to pull out of the Schengen passport-free zone unless other members do more to curb immigration from non-European countries.
Mr Hollande, for his part, has promised to raise taxes on big corporations and people earning more than 1m euros a year.
He wants to raise the minimum wage, hire 60,000 more teachers and lower the retirement age from 62 to 60 for some workers.
If elected, Mr Hollande would be France's first left-wing president since Francois Mitterrand, who completed two seven-year terms between 1981 and 1995.
If Mr Sarkozy loses he will become the first president not to win a second term since Valery Giscard d'Estaing in 1981.
French presidents are now elected for five years.
Frustration Wages, pensions, taxation, and unemployment have been topping the list of voters' concerns.
But the candidates have been accused of failing to address the country's problems during a lacklustre campaign.
Frustration with Mr Sarkozy's flashy style and with Mr Hollande's bland image has also allowed radical candidates to flourish.
Marine Le Pen, a media savvy far-right leader, has invigorated her anti-immigration National Front.
Meanwhile Jean-Luc Melenchon, who is supported by the Communist Party, has galvanised far-left voters.
Centrist leader Francois Bayrou is standing as a presidential candidate for the third time. In 2007, he came third, with nearly 19% of the vote.
Voting was held on Saturday in France's overseas territories - including Martinique and Guadeloupe in the Caribbean, Reunion Island in the Indian Ocean and French Polynesia.
Those territories vote early because results will be known on Sunday evening in mainland France - when it is still mid-afternoon in Caribbean islands and other overseas territories.
The presidential vote will be followed by a parliamentary election in June.

Saturday, April 21, 2012

Wazazi wa Kanumba sasa wavutana mgawo wa mali





WIKI mbili baada ya kifo cha aliyekuwa msanii nyota wa filamu nchini, Steven Kanumba, wazazi wake; Charles Musekwa Kanumba na Mama yake, Flora Mutegoa ambao hawaishi pamoja, wametofautiana kuhusu suala la mali na mirathi.
Juzi, Mzee Kanumba aliibuka na kudai kuwa kuna kundi la watu linalomdanganya mama huyo wa marehemu kwamba linajua zilipo mali za Steven jambo ambalo alisema ni uongo na kumtaka awe na subira na asidanganyike.
Hata hivyo, kauli hiyo imepingwa na Mutegoa ambaye amehoji sababu za mumewe huyo kuzungumzia mali za mwanaye wakati huu. Alidai kuwa Mzee Kanumba hajawahi kuwa na mawasiliano na marehemu tangu mwaka 1999 alipoondoka kwao, Shinyanga.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na gazeti hili juzi, Mzee Kanumba alimsihi mkewe kutodanganyika kwa kuwa yeye akiwa baba mzazi wa Kanumba anajua mali zote za mtoto wake na ndiye pekee anayeweza kumtendea haki katika kuzigawa.

“Mali za marehemu mwanangu nazifahamu zote, kwa hiyo hakuna shaka tutazigawa kwa sababu hakuna baba mwingine na haki yangu ipo palepale hakuna atakayeinyang’anya,” alisema na kuongeza:
“Nisingependa tuwape watu faida ya kuanza kuvutana mahakamani, tunatakiwa suala hili tulimalize sisi wenyewe kama tulivyompata mtoto wetu. Ninasisitiza mali zote zisifanyiwe vurugu ziachwe kama zilivyo.”
Katika kuthibitisha kwamba anazijua mali hizo, mzee huyo alisema Steven ameacha magari matatu, Sh40 milioni, viwanja viwili na akaunti mbili za benki na Kampuni ya Filamu.

Akerwa na tambiko
Mzee Kanumba alisema anasikitishwa na tambiko la Kihaya lililofanyika katika kaburi la mtoto wake, jambo ambalo alisema halikutakiwa kwa kuwa marehemu alikuwa Mkristo na alizikwa kwa imani hiyo.
“Mimi ni Mkristo, mtu aliyezikwa Kikristo huwezi tena kuanza kumfanyia mambo ya kipagani na kuanza kumtambikia, hiyo kwetu hairuhusiwi,” alisema Mzee Kanumba na kuongeza:
“Hata hivyo, marehemu alikuwa Msukuma, si Mhaya, itakuwaje wamtambikie Kihaya na kumwaga pombe aina ya rubisi huku marehemu alikuwa hatumii pombe na mimi pia situmii pombe?”
Kuhusu tambiko, Flora alisema hakuna kitu kama hicho kilichofanyika kwenye kaburi la mwanaye isipokuwa Wahaya wana mila zao kwa mwenzao aliyepatwa na msiba.

“Kilichofanyika siyo tambiko bali, ni mila zetu za Kihaya. Unapofiwa wenzako wanakuletea vitu kama kreti ya soda, bia na mkungu wa ndizi. Lile siyo tambiko ni mila tu, mimi pia ni Mkristo, siwezi kushiriki matambiko,” alisema.

Alisema suala hilo la kugawa mali au msimamizi wa mirathi walitakiwa kukutana pande mbili, yaani yeye na mkewe baada ya kupita siku 20 tangu alipozikwa waangalie namna ya kugawa huku akisisitiza kuwa hakuna mtu mwingine anayeruhusiwa kuingilia masuala hayo.

Mama amkana
Kwa upande wake, Mutegoa ambaye sasa bado yupo nyumbani kwa Kanumba, Sinza Vatican, Dar es Salaam alisisitiza kwamba marehemu hajawahi kuwasiliana na baba yake huyo tangu mwaka 1999.

Alieleza kushangazwa na taarifa hizo kutoka kwa mzazi mwenzake huyo na kusisitiza kuwa ni mapema mno kuanza kujadili mali za mtoto.

“Nasikitika kulisema hili kwani bado niko kwenye msiba wa mwanangu. Hata hivyo, sidhani kama mwenzangu anajua chochote kuhusu Steven, achilia mbali mali zake, hawajawahi kuwa na ukaribu mpaka kuweza kujua mali zake,” alisema na kuongeza:

“Hata hivyo, mbona anazungumzia mali tu, hivi anafahamu kama Steven alikuwa na madeni? Ninamsihi aachane na hizo habari kwa wakati huu kwani hazina uzito wowote ukilinganisha na thamani ya mtoto niliyempoteza,” alisema.
HABARI KWA HISANI YA GAZETI LA MWANANCHI
ba
Lucy