Ndugu
Ridhwan J. Kikwete akichangia jambo juu ya taarifa ya mapendekezo ya
kamati ya Uboreshaji wa Jumuiya ya umoja wa vijana wa chama cha
mapinduzi (CCM)
Mwenyekiti
wa Kamati ya Maboresho na Uimarishaji wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM) Ndugu Hussein Bashe akiwasilisha Taarifa ya
Mapendekezo ya kamati yake.
Katibu
Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Martin
Shigela, akielezea jambo juu ya mapendekezo ya Kamati ya maboresho.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Benno Malisa, akifafanua jambo katika kikao hicho.
Naibu
Katibu Mkuu (bara) wa Jumuiya ya umoja wa vijana wa chama cha
mapinduzi (CCM) akifafanua jambo katika kikao hicho cha kujadili
maboresho ya umoja huo.
Wajumbe wakifuatilia taarifa ya kamati kwa umakini.
---
Vikao
hivyo ambavyo vilianza rasmi tarehe moja June 1, 2012. ambapo hoja
mbalimbali zimekuwa zikijadiliwa kwa kina, ambapo vikao vilivyotangulia
vimejadili juu ya hoja ya Katiba Mpya na suala la Muungano wa
Serikali ya Jamhuri ya Muun gano wa Tanzania. Ambapo wajumbe
walichangia hoja mbalimbali za msingi kwa kuzingatia hali ya sasa ya
siasa nchini na matukio sambamba na hoja hiyo, kama vile mijadala
ndani ya majukwaa mbalimbali juu ya muundo wa Katiba ya sasa,
mapungufu yake na mchakato mzima wa kupata Katiba Mpya na pia mijadala
juu ya maboresho ya Muungano.
Pamoja na hayo, kikao kiliadili juu ya mapendekezo ya jinsi ya kuimarisha na kuboresho Umoja huo wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Mapendekezo
hayo juu ya jinsi ya kuboresho umoja huo yametolewa na Kamati maalum
ambayo ilipewa jukumu la kupendekeza namna ya kuiboresha UVCCM katika
kikao cha Baraza hili kilichokaliwa mnamo tarehe 19/03/2011, ili iweze
kukidhi mahitaji ya Siasa za ushindani wa sasa na baadae.
No comments:
Post a Comment