KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi, CCM, Nape Nnauye akimbeba
mtoto Goodluck John wa shule ya awali ya Lutheran, iliyopo Melizine
nje kidogo ya mji wa Njombe, baada ya kumkuta mtoto huyo akiwa na
wanafunzi wenzake miongoni mwa watu waliokuwa wakisubiri msafara wa
wake kupita eneo hilo akiwa njiani kuingia mjini Njombe.
--
.Asema waliowashauri kuibuni wamewaingiza 'mkenge'
.'Movement for Change' yao nayo ni ya kuchangisha fedha si kuleta mageuzi
.Asema itawachukua miaka mingi kuwa chama cha kweli cha siasa
.'Movement for Change' yao nayo ni ya kuchangisha fedha si kuleta mageuzi
.Asema itawachukua miaka mingi kuwa chama cha kweli cha siasa
--
NA BASHIR NKOROMO, NJOMBE
KATIBU
wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi, CCM, Nape Nnauye
amewananga CHADEMA kwamba aliyewapa wazo la kuanzisha kauli mbiu ya
'Vua gamba vaa gwanda' amewaingiza 'mkenge'.
Alisema,
Chadema wameingizwa mkenge kwa kuwa inajulikana wazi kuwa kaulimbiu
hiyo ililianzishwa na CCM, kukisafisha chama kiondokane na mafisadi wa
aina zote, na kwamba kwa Chadema kuanzisha 'vua gamba vaa gwanda'
maana yake wanafanya kampeni ya kubembeleza watu wa aina hiyo
wasiotakiwa CCM na Tanzania kwa jumla wahamie kwao.
Nape
alisema hayo, jana wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara
uliofanyika katika kijiji cha Mlangali, wilaya ya Ludewa mko mpya wa
Njombe, akiwa katika ziara ya kikazi katika mikoa mbalimbali kuimarisha
uhai wa chama.
"Itakumbukwa,
CCM kwa kuwa ni chama halisi cha siasa kwa kutimiza sifa, kinaendelea
na mageuzi makubwa ya ndani, yanayoitwa 'Kujivua Gamba', ikiwataka wale
wote wanaojihusisha na ufisadi wa ina zote kuondoka ndani ya Chama.
Lakini Chadema kwa kujua au kwa bahati mbaya wameamua kupotosha maana
halisi iliyo wazi ya zoezi hili kwa kuanzisha operesheni eti ya 'Vua
Gamba, Vaa Gwanda'", alisema Nape na kuhoji;
"Je,
kwa maana hiyo Chadema kama wamedhamiria hivyo na siyo bahati mbaya,
wamemua kuutangazia umma wa Watanzania na dunia nzima kwamba wako
tayari kuwapa hifadhi mafisadi wa aina zote ambao ni tishio kwa ustawi
wa taifa letu la Tanzania, ili mradi tu wapate idadi kubwa ya
wanachama?".
Nape
alisema, kama Chadema wangetumia busara wangeanzisha operesheni 'Vua
Gamba vaa Uzalendo', kwa sababu hakuna ambaye angeshangaa, kwa kuwa
kinachosababisha watu kuwa mafisadi ni kutokana na kukosa uzalendo
ndani ya mioyo yao.
"Kumwambia
mtu avue nguo ya ina moja avae nguo ya rangi nyingine huo ni upuuzi,
maana aina ya nguo inaweza kuwa utambulisho tu, lakini haisaidii
kubadili wala kujenga tabia ya mtu kiasi cha kuachana na ufisadi akawa
mwadilifu na mzalendo kwa nchi yale toka moyoni, mtu anaweza kuivaa na
kuivua wakati wowote, lakini kama watu wakihimizwa kuvaa uzalendo
wakauvaa sawa sawa, watakuwa nao mioyoni mwao daima, na hawatauvua muda
wowote kama nguo", alisema.
Nape
alisema kutokana na hali hiyo Wana-CCM wadilifu wasiwe na wasi wasi
kuhusu 'magamba' yanayohamia Chadema, kwa sababu kwa kujiingiza katika
kuyaona 'magamba' ambayo yamekubuhu kwa ufisadi kuwa ni mtaji kwao sasa
chama hicho kinajichimbia kaburi.
"Wewe
umesafiri kwa muda mrefu na gari lako, ukaliona mwendo wake umeanza
kuwa wa ndivyo sivyo, ukaamua kuondoa oil chafu kusafisha injini, sasa
wakati unasafisha akatokea mtu kuikinga akidhani itamfaa, wewe una
hasara gani? si unamuacha tu akahangaike nayo?, alisema Nape.
Katika
mkutano huo ambao ulijaa watu licha ya kufanyika kijijini, Nape
aliponda operesheni iliyoambana na 'vua gamba vaa gwanda' ya 'Momement
for Change-M4C', akisema hiyo ni operesheni ya kukusanya fedha tu, wala
siyo ya kuleta mabadiliko kama Chadema wanavyodanganya watu.
Alisema,
ni operesheni ya kutafuta fedha, na ndiyo maana kila wanapoitangaza
operesheni hiyo, wanachangisha watu fedha ambazo baadaye huwa
wachangishwaji hawaambiwi ni fedha kiasi gani kimepatikana.
"Ukinunua
kitu ukahitaji fedha iliyobaki si unasema nipatie 'chenji' yangu? sasa
wananchi muwe macho, msidhani hiyo ni operesheni ya mabadiliko, ni
operesheni ya wanaharakati kutafuta fedha, maana hata wao walishakiri
kwamba Chadema ni chama cha harakati na sasa kinajaribu kujitoa kwenye
uana harakati kiwe chama cha siasa cha kutafuta kutawala nchi" alisema
na kuongeza;
"Lakini
nawahaapia, hawa watakuwa wanaharakati kwa muda mrefu sana,
itawachulua muda mrefu kuwa chama cha siasa kwa kuwa historia
inathibitisha kuwa makundi mengi ya harakati yalichukua miaka mingi
sana ndipo yakawa vyama vya ssembuse hawa,watakula fedha zenu mpaka
mtachoka", alisema Nape.
Nape
jana alitarajiwa kufanyika mikutano mingine ya hadhara katika mkoa wa
Njombe kabla ya kujerea Dar es Salaam kwenye maandalizi ya mkutano
mkubwa wa CCM wa wajumbe wa mashina, matawi na viongozi mbalimbali wa
CCM na wanachama, utakaofanyika kwenye viwanjan vya Jangwani, Juni 9,
2012.
No comments:
Post a Comment