Mgeni rasmi ambaye pia ni Mkuu mpya
wa Wilaya ya Dodoma Mjini Mh Leph Gembe akiingia Ukumbini huku
akisindikizwa na Mwenyekiti wa taasisi ya wanafunzi wanaosoma shahada ya
kwanza ya sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma(UDOMSSO) aliyemaliza muda
wake Bw Emmanuel Misungwi katika ukumbi wa veta uliopo Mkoani Dodoma
katika Sherehe ya kuwaaga mwaka wa tatu wanaosoma shahada ya kwanza ya
sosholojia ya chuo kikuu cha Dodoma (UDOM)
Mgeni rasmi ambaye pia ni Mkuu Mpya
wa Wilaya ya Dodoma Mjini (Wa Pili Kushoto) Mh Leph Gembe akiwa katika
Picha ya Pamoja na Baadhi ya Viongozi wa taasisi ya wanafunzi wanaosoma
shahada ya Kwanza ya Sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma(UDOMSSO) ambao
wamemaliza muda wao ambapo wa kwanza kushoto ni Mwalimu mlezi wa taasisi
hiyo Bw. Jeremiah katika sherehe ya Kuwaaga wanafunzi wa mwaka wa tatu
wanaosoma shahada ya kwanza ya sosholojia
Baadhi ya wanafunzi wa mwaka wa tatu
ambao wanasoma shahada ya kwanza ya sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma
Wakiingia ukumbi kwa staili ya kucheza kwaito katika sherehe ya kuwaaga
mwaka wa tatu iliyofanyika katika ukumbi wa veta uliopo dodoma mjini
Baadhi ya wanafunzi walioshiriki katika sherehe ya kuwaaga mwaka wa tatu iliyofanyika katika ukumbi wa veta uliopo mjini Dodoma
Mwenyekiti Wa Kwanza na Muasisi wa
taasisi hii ya wanafunzi wanaosoma sosholojia ya Chuo Kikuu Cha Dodoma
ambaye amehitimu mwaka 2011 Mh Ibrahim Bakari akitoa neno wakati wa
sherehe ya kuwaaga wanafunzi wa mwaka wa tatu katika sherehe
iliyofanyika katika ukumbi wa veta
Makamu Mwenyekiti aliyemaliza muda
wake Bi Gaundensia Mwakemwa akimvalisha kitambulisho Makamu Mwenyekiti
Mpya Bw Mtono Juma kama ishara ya kukabidhi madaraka kwa viongozi wapya
wa taasisi hiyo.
Mwenyekiti mpya wa taasisi ya
wanafunzi wanaosoma sosholojia ya chuo kikuu cha Dodoma Bw Edgar Kelvin
akimkabidhi zawadi mkuu wa wilaya ya Dodoma Mjini Mh Leph Gembe ambaye
pia alikua mgeni rasmi wa sherehe ya kuwaaga wanafunzi wa mwaka wa tatu
wanaosoma shahada ya kwanza ya sosholojia ya chuo kikuu cha Dodoma
Wadada safi kabisa wakiwa wamebeba keki tayari kwaajili ya kuikata
Wawakilishi wa wanafunzi walioitwa
mbele kwaajili ya kukata keki kutoka kushoto ni Mwanafunzi Loyce Haule,
Katikati ni Shabani Kambi na Mwisho kabisa Ni Beatrice Msami
Baadhi ya wanafunzi wa mwaka wa tatu
na viongozi waliomaliza muda wao wakipokea vyeti kutoka kwa mgeni rasmi
ambaye pia ni Mkuu Mpya Wa Wilaya ya Dodoma Mjini Mh Leph Gembe kama
ishara ya kutambua majukumu yao kipindi wakiwa katika nafasi za uongozi
Muda wa Maakuli huo
MWENYEKITI WA KWANZA NA MUASISI WA UNIVERSITY OF DODOMA SOCIOLOGY
STUDENTS ORGANIZATION(UDOMSSO) AMBAYE AMEHITIMU KATIKA CHUO KIKUU CHA
DODOMA (UDOM) MWAKA 2011 NDUGU IBRAHIM BAKARI (Wa kwanza Kushoto)
KATIKA PICHA YA PAMOJA NA AFISA HABARI WA UDOMSSO ALIYEMALIZA MUDA WAKE
JANA NDUGU JOSEPHAT LUKAZA KATIKA SHEREHE YA KUTUAGA MWAKA WA TATU
TUNAOSOMA SHAHADA YA KWANZA YA SOSHOLOJIA YA CHUO KIKUU CHA DODOMA
No comments:
Post a Comment