Wednesday, April 25, 2012

Ni Maafa,Ubakaji, na Uasi DRC


Wanajeshi wa DRC wakimpa buriani mwenzao.

habari kutoka Mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo zinasema mapigano makali kati ya wanajeshi na waasi yamesababisha ubakaji wa halaiki na mauaji ya wanajeshi tisa.
Duru zinasema zaidi ya watu 100 wamebakwa katika eneo la Mweso lililoko Kivu ya Kaskazini. Zaidi ya raia elfu 80 wamaaninika kukimbia mapigano hayo ambapo pia kuna taarifa za wanajeshi 20 wa serikali kuasi.
Walioasi wanaaminika kuwa waaminifu kwa jenerali muasi Bosco Ntaganda anayetakikana na mahakama ya Kimataifa ya jinai-ICC. Ntaganda ameshtakiwa kwa makosa ya uhalifu wa kivita ambapo anatuhumiwa kuwasajili watoto jeshini.  habari kwa msaada wa BBC SWAHILI.COM

No comments:

Post a Comment