Katibu
wa NEC, Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa
habari Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, mtaa wa Lumumba, Dar es
Salaam, kuhusu maamuzi ya kikao cha Kamati Kuu ya CCM iliyokutana
mjini Dar es Salaam, ambapo pamoja na mambo mengine imeridhia Rais
Kikwete kuvunja Baraza la Mawaziri.
IFUATAYO NI TAARIFA ALIYOITOA KWA WAANDISHI WA HABARI.
Rais
amepokea taarifa na maazimio ya Kamati ya wabunge wa CCM na Kamati ya
uongozi ya wabunge wa CCM juu ya kilichotokea kwenye bunge lililopita
mjini Dodoma.
Taarifa hizo zimewasilishwa kwenye kamati kuu na kujadiliwa. Pamoja na
taarifa hizo kamati Kuu imepokea taarifa ya jinsi Rais alivyojipanga
kuchukua hatua za kuwawajibisha mawaziri na watendaji wa serikali na
wale wa mashirika ya umma waliobainika kuhusika na ubadhirifu
ulioinishwa na taarifa ya Mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za
Serikali, Kamati za kudumu za bunge na wabunge bungeni.
Kamati Kuu imeamua yafuatayo;
1. Kamati Kuu inatambua na kuheshimu haki na wajibu wa wabunge kujadili
utendaji wa serikali yao.Inapongeza juhudi za serikali kuhakikisha kuwa
ripoti ya mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali inajadiliwa
kwa uwazi na hivyo kuibua mapungufu yaliyojadiliwa.
2. Kamati Kuu imeridhika na imebariki uamuzi wa Rais KULISUKA UPYA
BARAZA LA MAWAZIRI na taasisi zingine zilizoanishwa katika ripoti hizo.
Imesisitiza utekelezaji wa uamuzi huo ufanywe mapema iwezekanavyo.
Aidha kamati Kuu imeipongeza Kamati Teule ya baraza la wawakilishi
Zanzibar iliyoundwa kuchunguza utendaji katika sekta mbalimbali kwenye
serikali ya mapinduzi Zanzibar kwa taarifa yao.
Kamati Kuu inawapongeza wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kwa jinsi
walivyojadili taarifa hiyo na pia Kamati Kuu inaipongeza Serikali ya
Mapinduzi Zanzibar kwa kuipokea taarifa na kuanza kuifanyia kazi.
No comments:
Post a Comment